Å·±¦ÓéÀÖ

Chuki Quotes

Quotes tagged as "chuki" Showing 1-10 of 10
Enock Maregesi
“Chukia kushindwa, zaidi ya unavyofurahia kushinda.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukitaka kumsahau mtu au kitu usimchukie au usikichukie kwa sababu kuchukia kuna nguvu sawa na kupenda.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Shetani hana uwezo wa kupandikiza chuki au upendo au kitu chochote ndani ya moyo wa mtu, bila mtu mwenyewe kupenda.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mfalme Sulemani alikuwa mtu mwenye hekima kuliko wote ulimwenguni. Anatushauri, “Adui yako akiwa ana njaa, mpe chakula; Tena akiwa ana kiu, mpe maji ya kunywa; Maana utatia makaa ya moto kichwani pake; Na BWANA atakupa thawabu (Mithali 25:21-22). Yesu anasema jambo fulani linalofanana sana na hilo katika mafundisho Yake yaliyofuata (Mathayo 5:44-45). Kitendo cha kutukanwa, kupigwa, kushtakiwa au kulazimishwa kubeba mzigo mzito usio wa kwako kinaweza kusababisha mafutu mabaya kabisa katika asili ya binadamu. Yaani, chuki, hasira, ukatili na hata vurugu. Lakini pale wale waliobarikiwa kuwa na hekima wanapojikuta katika majaribu makubwa kama hayo tabia yao haitakiwi kuwa ya shari, inda au ya kulipiza kisasi. Bali inatakiwa kuwa ya kusaidia, kuwa na ridhaa ya kutenda mambo mema, na kuwa mwema kwa wengine siku zote.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mshukuru sana mtu anayekuchukia, kwani chuki yake hukufanya mpiganaji.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Usimchukie mtu, chukia tabia yako.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kadiri unavyomchukia mtu mpende hivyohivyo.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukiichukia serikali yako umeichukia nafsi yako. Kwa sababu serikali ndiyo inayoongoza nchi, na nchi ni mwili mmoja.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kuipinga serikali si kuichukia; bali ni ombi la kutaka ibadilike.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Upendo ni daraja la chuki.”
Enock Maregesi