Å·±¦ÓéÀÖ

Maadili Mema Quotes

Quotes tagged as "maadili-mema" Showing 1-3 of 3
Enock Maregesi
“Wazazi wetu ni watu wa kuheshimu kuliko kitu kingine chochote kile kwa sababu wana uwezo wa kuona tusipoweza kuona. Yaani, wanajua kilichokuwepo kabla ya sisi kuzaliwa na wanajua kilichokuwepo baada ya sisi kuzaliwa. Maisha tuliyopitia, wazazi wetu walishapitia. Tulipokuwa, wazazi wetu walishakuwepo; na tulichofanya, wazazi wetu walishafanya. Hivyo, hatuna budi kuwaheshimu wazazi wetu. Lakini, wazazi wetu wanapaswa kujiheshimu kutufundisha adabu na maadili mema.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mwanampotevu dunia ilimfundisha ndiyo maana akarudi kwa baba yake akiwa amenyooka, hakuwa na maadili mema. Yusufu dunia ilimfundisha ndiyo maana akawa waziri mkuu wa Misri, na ndiyo maana akaokoa familia yake kutokana na njaa, alikuwa na maadili mema. Heri kudharaulika kwa kutenda mema kuliko kudharaulika kwa kutenda maovu. Ukidharaulika kwa kutenda maovu hutaishi sawasawa na mapenzi ya Mungu. Ukidharaulika kwa kutenda mema Mungu atakuinua.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Katika maisha, kila mtu ni kiongozi na ni mfuasi pia kutegemeana na hali. Kiongozi hatakiwi kuwa na kiburi, wala hatakiwi kuwa na roho yenye kutakabari, roho ya jeuri na kuona wengine si kitu, kwa sababu kiburi na roho yenye kutakabari huleta maangamizi na maanguko makubwa katika jamii. Viongozi wa mataifa wana jukumu kubwa kwa sababu kama wataruhusu maadili yaanguke, nguvu zao zote za kijeshi na kiteknolojia hazitawasaidia. Sifa ya kwanza ya kiongozi ni kuwa na maadili mema.”
Enock Maregesi