Å·±¦ÓéÀÖ

Kiburi Quotes

Quotes tagged as "kiburi" Showing 1-10 of 10
Enock Maregesi
“Mammon ni mungu wa pesa wa kuzimu anayesimamia mambo yote ya kifedha ulimwenguni. Ni miongoni mwa mashetani saba waliotupwa na Mwenyezi Mungu hapa duniani kutokea mbinguni akiwemo Ibilisi, Beelzebub, Asmodeus, Leviathan, Amon na Belphegor. Ibilisi ni mungu wa kiburi, Beelzebub ni mungu wa uroho, Asmodeus ni mungu wa zinaa, Leviathan ni mungu wa wivu, Amon ni mungu wa hasira na Belphegor ni mungu wa uvivu. Jukumu la mashetani hawa ni kusimamia kwa uaminifu mkubwa kutokea kuzimu dhambi kubwa saba duniani ambazo ni kiburi, uroho, zinaa, wivu, hasira, uvivu na uchoyo. Dawa ya dhambi hizo ni busara, kiasi, ujasiri, imani, haki, tumaini na upendo.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Wachawi wanamwabudu Shetani. Lakini Shetani wanayemwabudu si Shetani Ibilisi aliyeumbwa na Mwenyezi Mungu kuja kuudanganya ulimwengu wote. Ni Shetani roho ya mabadiliko, mabadiliko ya kweli, ya ufahamu kamilia ulimwengu huu ambamo sisi sote tunaishi. Wachawi, kwa maneno mengine, wanaabudu miungu â€� kama vile Inanna wa Mesopotamia, Isis wa Misri, Asherah wa Kaanani au Belus wa Assyria ambaye ndiye mungu wa kwanza kuabuadiwa kama sanamu duniani â€� iliyotwaliwa na Shetani tangu misingi ya ulimwengu huu kusimikwa. Dhambi aliyotenda Shetani mbinguni ni ndogo kuliko dhambi wanazotenda wachawi duniani, ijapokuwa dhambi aliyotenda Shetani haitaweza kusamehewa na ndiyo maana Shetani hataweza kuwasamehe wanadamu. Ni jukumu letu kuwaita wachawi wote kutoka Babeli na kuwaleta katika ukweli kama kweli wanayemwabudu ni Shetani Ibilisi, Shetani Beelzebub, Shetani Asmodeus, Shetani Leviathan, Shetani Mammon, Shetani Amon au Shetani Belphegor ambao ni mabingwa wa kiburi, uroho, zinaa, wivu, fedha, hasira na uvivu duniani. Wachawi hawajui, na usipojua waweza kufa bila kujua.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Katika maisha, kila mtu ni kiongozi na ni mfuasi pia kutegemeana na hali. Kiongozi hatakiwi kuwa na kiburi, wala hatakiwi kuwa na roho yenye kutakabari, roho ya jeuri na kuona wengine si kitu, kwa sababu kiburi na roho yenye kutakabari huleta maangamizi na maanguko makubwa katika jamii. Viongozi wa mataifa wana jukumu kubwa kwa sababu kama wataruhusu maadili yaanguke, nguvu zao zote za kijeshi na kiteknolojia hazitawasaidia. Sifa ya kwanza ya kiongozi ni kuwa na maadili mema.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Nisipopiga simu hupigi. Usipopiga sipigi. Hicho ni kiburi.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Usipojisajili BASATA watasema una kiburi. Serikali hupenda watu iliyoridhika nao. Wasanii wote nendeni BASATA mkajisajili.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Geuza kiburi chako kuwa hekima.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Bila kiburi hutamshinda Shetani, lakini kiburi dhidi ya Shetani unakishinda kwa hekima.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kabla hujatenda dhambi Roho ya Mungu itakwambia kwamba hiyo ni dhambi. Ukiitenda hicho ni kiburi.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Shetani hatawasamehe wanadamu kwa sababu ya kiburi.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Toba ina nguvu zaidi kuliko kiburi.”
Enock Maregesi