Å·±¦ÓéÀÖ

Si Jambo Rahisi Quotes

Quotes tagged as "si-jambo-rahisi" Showing 1-2 of 2
Enock Maregesi
“Msamaha si jambo rahisi. Tunapoumizwa, au watu wetu wa karibu wanapoumizwa, tendo la kusamehe linaweza kuwa gumu kuliko matendo yote. Lakini, tambua kwamba msamaha ni mchakato wa muda mrefu unaohitaji ujasiri mkubwa kuuanza hadi kuukamilisha, ongea na watu wanaoelewa maana ya msamaha ili wakuongoze katika mchakato huo. Vilevile, tambua kwamba hata wewe umewahi kufanya makosa na unahitaji msamaha, tambua kwamba suluhisho kamili linahitaji matendo kutoka kwa aliyekosea na kwa aliyekosewa. Wengine hupendwa kwa sababu wanastahili, lakini wengine wanastahili kwa sababu hupendwa. Mungu anatupenda kwa jinsi tulivyo hata kama tunajiona hatustahili. Hivyo, jithamini.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Shahidi mwaminifu na wa kweli anayajua mambo yetu yote tangu kuumbwa hadi mwisho wa dunia yetu. Kwa hiyo, ni kweli unabii lazima utimie. Mungu anataka tuwe na amani ndani ya mioyo yetu lakini anajua si jambo rahisi kwa sababu ya hila za Shetani. Shetani asingekuwepo amani ingekuwepo; watakatifu wasingekuwepo, dunia isingekuwepo. Lakini mlango wa rehema bado haujafungwa. Bado tuna uhuru wa kuchagua mema dhidi ya mabaya.”
Enock Maregesi