Å·±¦ÓéÀÖ

To Die Quotes

Quotes tagged as "to-die" Showing 1-5 of 5
“When you live.. You can die.. Accept it... ..and become fearless”
Erik Tanghe

Enock Maregesi
“Tunazaliwa na kufa. Lakini hatujui tunakotoka. Wala hatujui tunakokwenda. Huenda tunatoka na kwenda katika dunia nyingine, ya ulimwengu mwingine, hivyo kutufanya wageni wa dunia yetu wenyewe. Acha dunia katika hali nzuri kuliko ulivyoikuta.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Tunazaliwa, kuteseka na kufa kwa sababu ya dhambi ya asili ya wazazi wetu wa kwanza (Adamu na Hawa). Kama Hawa asingekubali kudanganywa na Shetani, tungezaliwa bila uchungu, tungeishi bila kuteseka na tusingekufa milele. Lakini haya ndiyo mawazo yangu: Mungu Ahusiki na dhambi, Ahusiki na mwili, Anahusika na roho. Hivyo, mtu anapofariki mwili unabaki duniani lakini roho inarudi kwa Mungu; kwani Yeye ndiye aliyeitengeneza na kuiweka katika moyo wa mtu. Mimi na wewe ni viumbe vyenye thamani kubwa sana mbele za Mwenyezi Mungu; mapenzi Yake kwetu hayana masharti yoyote. Hainiingii akilini (hata kidogo) kumtesa mtu unayempenda kiasi hicho milele, wakati uwezo wa kumwokoa unao.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Asiyeogopa kufa anaogopa kuishi.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Yeyote anayesema haogopi kufa anajua hatakiwi kuwa jasiri kiasi hicho.”
Enock Maregesi