Å·±¦ÓéÀÖ

Mateso Quotes

Quotes tagged as "mateso" Showing 1-3 of 3
Enock Maregesi
“Lakini damu na maji vina maana kubwa katika maisha yetu. Biblia inaeleza kuwa wakati Yesu Kristo akiwa msalabani alichomwa ubavu wake kwa mkuki, ikatoka damu na maji, ndipo zilipozaliwa sakramenti za kanisa. Aidha, tukio la askari wa Kirumi kumchoma Yesu na damu na maji kutoka lina maana nyingine kubwa katika maisha yetu. Hapo ndipo Ukristo ulipozaliwa; na ni kwa sababu hiyo mwanamke anapojifungua hutoa damu na maji kutokana na kupasuka kwa utando wa mfuko wa uzazi. Kutokana na hayo, Wakristo wanapoabudu msalaba wanaeleza umuhimu wa matukio na mafundisho waliyopata kupitia mateso aliyopata kiongozi wao na kuwa, msalaba ni chombo cha ukombozi.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Mateso yalishakuwa mengi, na Murphy alishakata tamaa. Kesho yake alitamani sana aione lakini hakukuwa na dalili yoyote ya maadui kumwacha hai. Walivyomning’iniza kama nyama ya kuokwa kwa kipindi kirefu, walichoka kupiga na kumkalisha katika kiti cha umeme na kumfunga miguu na mikono kwa machuma makubwa yaliyofanana na pingu.”
Enock Maregesi, Kolonia Santita

Enock Maregesi
“John Murphy alifanya mapenzi na Debbie kwa faida ya Tume ya Dunia.”
Enock Maregesi