Å·±¦ÓéÀÖ

Ukweli Quotes

Quotes tagged as "ukweli" Showing 1-19 of 19
Enock Maregesi
“Kama umefanya au umesema kitu kibaya na ukasema ukweli mbele ya mtu au ya watu, omba msamaha kupata tena kibali cha umma.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kama utafiti wa mtu umevuka mipaka ya ukweli au uhalisia toa utafiti mwingine kuupinga huo wa kwake, kwa lengo la kuelimisha wengi. Haina maana kusema jambo si la kweli na usitwambie kwa nini si la kweli.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Kujua ukweli juu ya uraibu wa madawa ya kulevya kunaweza kumsaidia mtu kujua madhara ya madawa ya kulevya.”
Enock Maregesi

Dora Okeyo
“You are the earth, my dear grandson, and just like it takes everything without complaining, so have you shown us today that you will take everything in kind, and there's no greater title than this.”
Dora Okeyo, Fire

Enock Maregesi
“Tunasema uongo kwa sababu hatuna ujasiri wa kusema ukweli. Ukweli hautupi uhuru, unatupa upweke.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukisema ukweli utapata uhuru wa nafsi. Ukisema uongo utapata uhuru wa umma. Heri uhuru wa nafsi kuliko wa umma.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Tupo watu takriban bilioni saba katika dunia hii. Kila mtu ni wa kipekee. Mathalani, wewe ni tofauti na baba yako au mama yako au mtu mwingine yoyote yule. Kila mtu aliumbwa kivyake na Mwenyezi Mungu. Kila mtu ana nafasi ya kwake mwenyewe aliyopangiwa na Mungu hapa duniani. Haijalishi wewe ni mwanamke au mwanamume, mweupe au mweusi, mfupi au mrefu, mzuri au mbaya, una nafasi katika nchi na dunia hii. Unachotakiwa kufanya ni kuamka, kufumbua macho na kuujua ukweli. Tafuta maarifa katika Biblia kama wewe ni Mkristo. Tafuta maarifa katika Kurani kama wewe ni Mwislamu. Tafuta maarifa katika Yoga kama wewe haumwamini Mungu. Ukishaamka na kuujua ukweli, ukishapata nafasi katika nchi yako, kuwa kiongozi na mkarimu kwa wenzako. Jifunze kutoka kwa wengine ndani na nje ya tasnia yako. Usiwe mchoyo wa maarifa. Kuwa mwadilifu. Ukifanya hivyo utafanikiwa zaidi, utaipa heshima tasnia yako, na utaacha alama katika dunia baada ya kuondoka. Kuacha alama katika dunia si lazima upate nafasi katika dunia. Kuacha alama katika dunia acha alama katika nchi yako.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Wachawi wanamwabudu Shetani. Lakini Shetani wanayemwabudu si Shetani Ibilisi aliyeumbwa na Mwenyezi Mungu kuja kuudanganya ulimwengu wote. Ni Shetani roho ya mabadiliko, mabadiliko ya kweli, ya ufahamu kamilia ulimwengu huu ambamo sisi sote tunaishi. Wachawi, kwa maneno mengine, wanaabudu miungu â€� kama vile Inanna wa Mesopotamia, Isis wa Misri, Asherah wa Kaanani au Belus wa Assyria ambaye ndiye mungu wa kwanza kuabuadiwa kama sanamu duniani â€� iliyotwaliwa na Shetani tangu misingi ya ulimwengu huu kusimikwa. Dhambi aliyotenda Shetani mbinguni ni ndogo kuliko dhambi wanazotenda wachawi duniani, ijapokuwa dhambi aliyotenda Shetani haitaweza kusamehewa na ndiyo maana Shetani hataweza kuwasamehe wanadamu. Ni jukumu letu kuwaita wachawi wote kutoka Babeli na kuwaleta katika ukweli kama kweli wanayemwabudu ni Shetani Ibilisi, Shetani Beelzebub, Shetani Asmodeus, Shetani Leviathan, Shetani Mammon, Shetani Amon au Shetani Belphegor ambao ni mabingwa wa kiburi, uroho, zinaa, wivu, fedha, hasira na uvivu duniani. Wachawi hawajui, na usipojua waweza kufa bila kujua.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Pambana na Shetani kwa upanga wa imani ambao ni ukweli kwani ukweli ndiyo utakaokuweka huru.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Utajiri una changamoto nyingi. Yesu alisema ni rahisi kwa ngamia kupita katika tundu la sindano kuliko tajiri kuingia katika ufalme wa Mungu. Hakusema msomi. Usiwe mwendanguu. Jikusuru kuujua ukweli.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Lakini ukweli ni upi? Ukweli ni kwamba utajiri una changamoto nyingi kuupata na kuudumisha pia kuliko usomi na kwamba ukweli ni amani ya Mungu katika moyo wa mwanadamu. Heri msomi kuliko tajiri â€� Heri yule aliyesoma kuliko tajiri asiyesoma au yule aliyesoma kuliko vile alivyosoma tajiri au tajiri asiyesoma au aliyesoma lakini asiyekuwa na tamaa kabisa na dunia hii ambaye kukosa kwake tamaa na dunia hii kunamfanya msomi. Ndivyo Kristo anavyomaanisha. Si kwamba tajiri hawezi kuuona ufalme wa mbinguni. Ibrahimu, Isaka, Yakobo, Yusufu, Daudi, Sulemani, Yehoshafati, Hezekia, Zakayo, Yoana, Susana, na Lidia watauona ufalme wa mbinguni na walikuwa matajiri. Mali zao zilivyozidi hawakuangalia moyoni, hawakuwa na tamaa kabisa na dunia hii, bali walimtumaini Mungu kwa kila kitu walichokuwa nacho. Anaweza. Lakini asiipende dunia bali ayapende mambo ya ufalme wa Mungu kwa moyo wake wote.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukweli unauma na unaumiza!”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukitaka kuchukiwa sema ukweli!”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukweli unauma na unaumiza.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Hakuna kitu kizuri hapa duniani kama ukweli.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Ukiujua ukweli unaridhika moyoni.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Siwaogopi wenye dhambi ndiyo maana ninawafundisha ukweli.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Neno la Mungu tunalojifunza sasa litatufanya tuusimamie ukweli, uliodhihirishwa na mitume, katika kipindi cha dhiki kuu.”
Enock Maregesi

Enock Maregesi
“Manabii wa uongo, na wafuasi wao, hawautaki ukweli. Kazi yao ni kutulazimisha tumwabudu Mpinga Kristo, badala ya Yesu Kristo, bila sisi wenyewe kujua. Wana mamlaka yote ya Mpinga Kristo kwa sababu, kama Mpinga Kristo, wanaongozwa na Shetani. Walimu hawa wa uongo wanaopenda kuvalia misurupwenye ya kisawasawa, na wanaoongea utafikiri wamemeza Biblia na kuitapika kwenye mikrofoni, lengo lao ni kutupeleka kwenye ufalme wa Shetani. Hatuna budi kuitangaza injili ya kweli ya Yesu Kristo, kwa imani ya kweli, kupata urithi usiohongeka wa ufalme wa Mungu.”
Enock Maregesi